Saturday, February 16, 2008

Baraza la Mawaziri Tanzania

Hii ni Kasi Mpya Ari Mpya na Nguvu Mpya


Naufurahia msemo huu kwani kasi mpya haiwi tu kwa maneno lazima iwe pia kwa vitendo ili iwezekuthibitika. Nguvu mpya lazima mtu ajue kuvumilia magumu na halafu anaibuka na nguvu mpya katika kukabiliana na jambo lingine, Ari mpya inatukumbusha kutokata matumaini, kila kitu kinauvumbuzi hakuna tatizo lisilo na mwanzo wake, na hakuna Hesabu isiyo na Jibu, vile vile ukizaliwa kumbuka kwamba kunakufa. Ikiwa ulisifiwa kataka jambo furani kumbuka kutunza heshima ya sifa uliyopewa, ukijisahau yatakukuta haya mabadiliko yasiyokusudiwa. Lakini ili tusonge mbele hatuna budi kutolea sadaka walio makafara.

Mimi naongea na Mh. Jk na kumwuliza maswali kadhaa na yeye anajibu kama ifuatavyo:-

Mwadishi. Mbona sura nyingine sizioni?
Jk. Wameomba kupumzika!
Mwandishi. Mbona wengine wanalia kama wameomba kupumzika kwa hiari?
Jk. Hao wanaolia wanayao!
Mwandishi. Umeamua kumwaga na rafiki yako wa damu?
Jk. Alikuwa anajibu kuchezea shilingi chooni alifikiri haitatumbukia, umeona mwenyewe kilichofanyika!!
Mwandishi. Yaani ndo kusema umeamua kufanya kweli mzee?
Jk. Ili maandiko ya timie haina budi wengine kutolewa kafara, na mimi nimetolea kafara kondoo wangu, ili mjue kuwa ninauchungu na Ninyi Watanzania.
Mwandishi. Mimi nilifikiri unatania kumbe kweli?
Jk. Ulisha wahi kukamata kisu kwenye makali harafu usikatwe, au unategemea nini kama unachezea moto?

Mwndishi. Mzee tutakufa njaa ?
Jk.
Kama uligundua kwamba utakufa njaa ungefanya kazi kwa bidii na maarifa ili uwe na uhakika wa kupata Unga wa kesho. Kumbuka njia ya mkato ni nzuri na ina hasara zake, sasa unalilia nini, haya yaliyotukia uliyataka mwenyewe kwani hukujua kama unaiba?
Mwandishi. Mimi nilikuwa najaribu tu nione kama utagundua ...... nani ....
Jk. Sijazaliwa leo kwa heri ......
Mwandishi. Amaa kweli nilitegemea nitafichwa na wenzangu kumbe ndiyo wamenianika sasa mimi nitakuwa mgeni wa nani?


Baraza la Mawaziri


How to make a woman Happy

Mfanye mwanamke awe na furaha kwa kutekeleza hayo! Swali ukisha mtekelezea atakulinda? je hamu yake ya kutaka vinavyojitokeza kila siku itamwisha? Je, kwa uchumi wangu huu nitaweza au nimwache? Jibu mtihani huu katika maisha usione so!




WITHOUT FORGETTING TO:

44. give her compliments regularly

45. love shopping

46. be honest

47. be very rich

48. not stress her out

49. not look at other girls






HOW TO MAKE A MAN HAPPY :


provide him with
1. Good food;
2. Sex

Usawa upo wapi??????????????


Tunza Mazingira ni Uhai

Ndugu yangu mazingira yanalindwa na sisi sote si jukumu la serikali wala mgambo kulinda mazingira. Kwani ukilinda mazingira ni sawa na kuulinda uhai wako. Mazingira ni uhai, kutokana na mazingira kuwa katika hali nzuri tunapata mvua, na mvua inafaida nyingi. Tunapata maji ya kuzalishia Umeme, na pia tunatumia maji haya haya katika umwagiliaji wa mashamba na si hayo tu, tunapata maji safi kutokana na kutunzwa vyema kwa mazingira na vyanzo vyake. Je, unapokata miti unafikiria haya yote, au unatafuta faida yako binafsi, na ninyi mnaotengeneza mkaa kwa kukata miti ovyo kweli mnaharibu mazingira kwa asilimia kubwa sana, hivi mnajua au mlikimbia shule kwa sababu ya kuogopa umande? Matokeo yake ndiyo haya sasa mnashindwa kuchambua lipi la msingi na lipi linahasara kubwa kwa jamii, ndugu yangu nakushauri Elimu haina mwisho nenda kasome sasa na ujue faida za mazingira.

MLIMA KILIMANJARO

Kivutio mojawapo mhimu Tanzania

MILIMA YA ULUGURU KUTOKEA STENDI ZA MABASI YA HOOD HOOD MJINI MOROGORO
MTO RUAHA UNAOTENGANISHA MKOA WA MOROGORO NA IRINGA





Picha kwa uhisani wa blog ya kaka Michuzi


Picha kwa hisani ya blog ya Ngurumo


Kivutio kikubwa cha Nchi yetu.

Wednesday, February 13, 2008

Je, kumshukuru Mungu ni jambo la lazima au lahiari?

Mpendwa, nimeweka swali hapo juu kwa makusudi mazima ili tuweze kuingia ndani ya mioyo yetu na kujichunguza, kwa kina kama kumshukuru Mungu ni jambo la hiari au unawajibika kumshukuru.

Kwa mimi binafsi nimejionea mambo mengi ambayo kwa mimi peke yangu bila uwezo wake mola nisingeliweza kuyatekeleza, hivyo basi nikatafakari kwa kina na nikatoa uamuzi wangu kuwa kwangu mimi kumshukuru Mungu kwa kila dakika ninayopewa ni wajibu. Ameniokoa katika mambo mengi na bado anaendelea kunilinda, sasa kwa nini nisimshukuru, na tena hajaniokoa tu bali amenisaidia wakati wa shida kujua njia ya kupita.


Nikusimulie yaliyonikuta kwenye mtihani, nilikuwa sijui kabisa baadhi ya maswali na mwalimu aliruhusu kumwuliza pale ambapo unahisi kunatautata katika kuelewa swali. Wenzangu waliuliza akawaelekeza na mimi nilipomwuliza akasema haelewi, kile nilicho mwuliza lakini haikuwa kweli kwamba haelewi alikuwa anafahamu lakini hakutaka kuniambia basi katika muda kama huu ndiyo unapojua kwamba miujiza ya Mungu inafanya kazi, mimi nilijibu vile nilivyo hisi kwamba linaweza kuwa jibu sahihi, ni kweli nilipata majibu ambayo mimi mwenyewe kwa uwezo wangu sikuya jua kabisa.

Ndipo nilipoamini kwamba Mungu hana hiana kwa wale wanaomwamini. Wewe mwenzangu je! Na wengi wetu tunakuwa na imani na Mungu hasa wakati tunapokabiliwa na shida kama mitihani, tunategemea kwamba Mungu afanye miujiza ili tufaulu, na wengine wetu ndo hawa somi kabisa wanategemea miujiza ya Mama Bikira Maria, katika dakika hizi za mwisho, na kwamba huko nyuma wala hawa kuwa wanajishughulisha naye kabisa.

Ndugu yangu huko ni kutaka kumkamua Mungu na Mama yetu Bikira Maria miujiza, kumbe busara ya kweli ni hii ya kujisaidia nami nitakusaidia, soma nami nitakusaidia pale ambapo umeshindwa kabisa.

Mshukuru Mungu kwa kukupa Afya njema

Tunakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutujalia zawaidi ya kuwa na afya njema, na hata uzuri tulionao, kama hufanyi hilo unamkosea haki Mungu wako aliyekuumba.

Nami nakuuliza swali je hawa walisitahili kupata haya, bila shaka jibu ni hapana, je kwa nini sisi tusimshukuru kwa zawaidi ya uhai tuliojaliwa?

Habari ya kusikitisha zaidi mwaka 2007












Monday, February 11, 2008

Love Love Love

Je, bila upendo unaweza kuishi? Bila shika kila mmoja wetu anajibu tofati kadiri ya tafsiri ya neno Love au Upendo lilivyo. Basi niwape nafasi kutafuta ukweli upo wapi.

How would you respond to someone who comes infont of you and says I L O VE you?

It is very simple to answer this Question Just say to her, Thank You, I LOVE you too. You guys don't think too much, you will loose more Kilokarolies while the Lady just ment to say she loves you the way you are.

Look down what do you see!
That is Love. We were Created by God to Love each other, do you do the same or you are looking for something else?



Mpendwa msomaji wangu, mmoja alipata kigugumizi kidogo akaamua kuniuliza moja kwa moja, kwamba anashindwa kufikia uamuzi wake wa kutaka kuishi na mwandani wake, kwa kuwa mwili moja.

Na mimi nilimshukuru kwa kufikia uamuzi huu, kwani mara nyingi tumeingia pupa katika fani na hatimaye tunajikuta tunaangukia pua. Naomba uambatane nami katika kuyachambua haya machache :-

Mambo mhimu ya kuzingatia

  • Mchague mtu ambaye unauhuru wa kuongea naye
Wengi wamekuwa wakipotea njia na kuchagua watu ambao sio matamanio yao wala hawafurahii kuongea nao, kuongea ni sanaa ambayo inahitaji ufundi na ujuzi kama fani zingine katika kupanga maneno na kupendezesha au kunogesha mazungumzo. Matokeo yake wakisha kaa kama mme na mke, mme anaamua kurudi nyumbani kwa kuchelewa akisingizia kazi nyingi. Lakini ukweli ni kwamba nyumba imeingi Luba, hakuna maongezi ya kunogesha upendo wenu.
  • Mchague mtu mnayeendana kitabia au walau kulandana katika mambo fulani
Hii itakupa furaha kwani muda mwingi ambao mtakuwa pamoja utapenda kusikia mawazo yake na kusikia kipya toka kwake. Na hii itadumisha upendo baina yenu.
  • Uwe sababu ya yeye kuwa na furaha
Hapa nataka kumanisha kuwa naomba uepukane na vitu ambavyo vitakuwa hatarishi kwa uhusiano wenu.
Kwa mfano: kuwa chagua marafiki wenye tabia zuri, kutawafanya muwe na furaha kwani kesi za mara kwa mara na marafiki zenu hazitakuwepo.

-Hakutakuwa na kuingiliana Nyumba

-Hakutakuwa na masengenyano yasiyo na vichwa wala miguu

-Hakutakuwa na kuchuguzana leo jirani anakula mboga gani au amevaa nguo ya aina gani
  • Muwe watu wa furaha
Utashangaa kuona watu wanaishi nyumba moja ila wanajifunika shuka tofauti, hasa kwa nini kuusemea moyo? Hujui kwamba huyo ndiyo wako mpaka mauti yatakapo watenga, na kama leo unafanya hivi, si unampa jibu kwamba nenda kungine kwangu ulipotea njia?
  • Shirikishaneni matatizo yanayowapata katika maisha
Ukifanya hivi kila mmoja atamjali mwenzake kwani hakutakuwa na kutiliana mashaka katika uhusiano wenu.
  • Pakitokea mtafaruku wa mawasiliano baina yenu kaeni chini muongelee tofauti zenu
Kuzungumzia tofauti baina yenu kutawafanya mjenge mahusiano mazuri na ya kuaminiana, naomba nikuulize swali, wangapi leo wanakaa na wake zao au waume zao na kuwauliza kwa upole juu ya mapungufu waliyoyasikia? Na unachukua uamuzi gani baada ya kusikia hayo kutoka kwa mwenzi wako?
  • Usipende kuamini kila unaloambiwa na watu juu ya yule unayempenda, au mwenzi wako
Tumia muda mwingi kumsoma mpendwa wako kabla hujafikia uamuzi wa kumfanya awe mwenzi wako. Ni nafasi mhimu sana kufahamiana, bila hilo migongano mingi itajitokeza. Na sababu yake ni kwamba hukuwa makini mwanzoni wakati unafanya uamzi wako.

Jaribu kuutafuta ukweli wa jambo kabla ya kufikia maamuzi, jambo ambalo umekusudia kulitekeleza.


  • Usimtendee mwenza wako jambo ambalo wewe usingependa kutendewa
Kitu kinginne cha msingi hapa ninachotaka wote kutambua ni kwamba, usimtendee mwenza wako (mke wako) jambo ambalo wewe usingependa kutendewa. Na ikiwa limetukia kwa ajali, binadamu ndiye binadamu, basi ni vema kumwomba radhi mwenza wako tena kwa adabu. Kumbuka kwamba haya hayapatikani kwa kila mtu ila kwa wanaume wachache wanaomjua Mungu, na si tu kumjua Mungu bali pia awe ni mtu anayejishughulisha na mambo ya Kanisa hii itakuwa kama chachu ya yeye kukuza uhusiano wake na Mungu na wako pia.

Mwisho Maandiko Matakatifu yatufundisha jinsi ilivyo vema kwa ndugu kuishi kwa moyo moja na roho moja. Kutatupunguzia magonjwa ya moyo, ambayo tunakutana nayo katika maisha.

Sunday, February 10, 2008

Mheshimiwa Jk na Waziri Mkuu Pinda

Waziri Mkuu mpya akiwa katika pozi na Mheshimiwa Jk, kichwa cha watanzania bara na visiwani, katika kuhakikisha maisha bora kwa watu wote. Swali langu ni hili Je, ndoto yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania itatimia?

Bega kwa bega

Saturday, February 9, 2008

Busara ya Lowasa

Ingawa watu wanamwona kama kakosea na huenda ameidhalilisha Serikali, kwa upande mwingine amefanya jambo la busara sana, kujitoa katika madaraka ili mwingine ashike nafasi yake. Wengi hasa waliomadarakani huwa hawawezi kujinyenyekesha hivi, ila huyu ameweza kufanya ili kutunza heshima ya Serikali na ya viongozi wenzake. Tuige mfano wake, kwa kuweza kujishusha bila kujali kupoteza heshima zetu katika jamii. Bila Hekima hii ya kukubali kushindwa, yangetukuta ya watu wa Kenya, kuanza kuchinjana kama wanyama, sababu ni nini, jambo la kwanza ni kutokukubali mabadiliko kwa sababu ya masilahi ya Tumbo langu, na sio maisha mazuri kwa kila mtu.

pongezi


Waziri mkuu mpya mh. pinda akipongezwa na waziri mkuu aliyepita kabla yake mh. lowassa mara bada ya kuapishwa leo ikulu ndogo ya chamwino, dodoma