Wednesday, August 12, 2009

Maisha ni safari

Namshukuru Mungu kunifikisha hapa nilipofikia, naamini kwamba bila huruma yake nisingeweza kufikia hapa nilipofikia. Hai manishi kwamba nimefauru kufikia kikomo cha maisha, lakini walao hatua fulani katika maisha nimeweza kuifikia.
Mungu mwenye rehema na upendo ahimidiwe.
Siku ya leo nimejifunza yafuatayo:-
  • Katika maisha yako hapa duniani usimwamini binadamu mwenzio hatasiku moja, jiamini wewe na Mungu wako.
  • Ukimtegemea mtu usiyemfahamu atakuua bila kujifahamu.
  • Usione mtu anacheka mdomoni ukafikiri na Rohoni ni vivyo hivyo.
  • Mwanadamu ni kiumbe geugeu sana
  • Umdhaniae ndiye kumbe siye.

Mungu mwenye huruma na Mapendo atujalie nguvu na mshikamano tuendelee kujifunza nini maana ya maisha na sio kukata tamaa.